Shared teaching resources for category: LMS Training
ENG 2223: Introduction to Phonetics and Phonology SEP - DEC 2025
GEO 4135: Human Settlements and Statistics SEP - DEC 2025
KSW 4153: Mbinu za Utafiti katika Lugha na Fasihi SEP - DEC 2025
KSW 1123: Utangulizi wa Fasihi Katika Kiswahili SEP - DEC 2025

KAG EAST UNIVERSITY
UTANGULIZI WA FASIHI KATIKA KISWAHILI
KSW: 1123
MUDA WA KIPINDI: SAA 3
MHADHIRI: EMMAH ACHIENG
NAMBARI YA SIMU: 0790982044
BARUAPEPE:emmah.achieng@east.ac.ke
MADHUMUNI YA KOZI
Kozi hii inalenga kumpa mwanafunzi nafasi ya kuielewa fasihi. Kozi itazingatia kwa jumla mambo ya kimsingi yanayohusiana na taaluma ya fasihi. Lengo maalum ni kuhakiki na kuchanganua mbinu mbalimbali za fasihi kwa kuzingatia tanzu mbalimbali za fasihi.
Kozi hii itachangia katika kutimiza malengo ya CHUO KIKUU CHA KAG MASHARIKI kwa sababu inahusiana na chuo hiki kama taasisi ya elimu. Kila mwanafunzi anatarajiwa kutimiza malengo ya taasisi hii atakapokuwa akifanya kazi katika sehemu mbalimbali za kazi.
CHUO KIKUU CHA KAG MASHARIKI ni taasisi ya Kipentekoste inayodhamiria kuwaandaa viongozi watumishi watakaoleta mabadiliko chanya kote duniani kwa kuishi maisha mema na kufanya huduma inayoongozwa na Roho Mtakatifu.
Malengo ya Kozi
Kufikia mwisho wa kozi hii mwanafunzi aweze:
1. Kupambanua dhana ya fasihi kwa jumla
2. Kutathmini umuhimu wa fasihi katika jamii ya kisasa.
3. Kubainisha tofauti zilizoko za umbo na mtindo katika nyanja / tanzu za fasihi
4. Kuhakiki vipengele muhimu katika tanzu za fasihi kama aina za riwaya, tamthilia, ushairi, ploti, vitushi, arudhi, jukwaa, wahusika, tamathali za usemi na kadhalika.
5. Kujadili mwingiliano uliopo kati ya tanzu na vijitanzu vya fasihi ya Kiswahili.
6. Kuchambua kazi za fasihi ya Kiswahili.
7. Kutafiti aina za fasihi zinazopatikana katika jamii yake.
MAELEZO
Dhana ya fasihi; maana ya fasihi; chanzo cha fasihi; vipengele vya fasihi; fasihi simulizi: maana yake, tanzu na vipera vyake; fasihi andishi: riwaya, maana ya riwaya, historia ya riwaya, aina za riwaya, fani na maudhui katika riwaya/dhamira, uchambuzi wa riwaya; hadithi fupi: maana ya hadithi fupi, fani na maudhui; tamthilia: maana ya tamthilia, historia ya tamthilia, uhakiki wa tamthilia; ushairi: maana ya ushairi, historia ya ushairi, aina za ushairi, uchambuzi wa ushairi.
Kama taasisi ya Kikristo ya elimu ya ngazi za juu CHUO KIKUU CHA KAG MASHARIKI inashughulika mno na kujenga mtazamo wa Kikristo kuhusu elimu. Katika chuo kikuu hiki, Ukristo uliomo katika biblia ndio msingi wa mpango mzima wa elimu au mkondo ambao mto wa kufunza na kusoma unatiririkia. Kwa hivyo, ni jukumu la mhadhiri kuwapa wanafunzi mitazamo ya biblia katika kila somo na zoezi. Kwa maneno mengine, kuambatisha biblia na elimu kunahitajika.
|
JUMA |
MADA |
MADA NDOGO |
MALENGO |
UMILISI |
SHUGHULI ZA MHADHIRI |
SHUGHULI ZA WANAFUNZI |
|
1 |
Dhana ya fasihi |
Fasili mbalimbali za Fasihi
Chanzo cha fasihi |
LENGO 1 |
Uwezo wa mawasiliano na ushirikiano(wanafunzi wanapojadiliana na wenzao na kutoa fasili mbalimbali za fasihi) Ujuzi wa kidijitali(ywanapotafuta fasili mbalimbali za fasihi mtandaoni |
Kuuliza maswali kuhusu fasili mbalimbali za fasihi
Kuwaeleza wanafunzi kuhusu chanzo cha fasihi |
Kuandika
Kujadiliana na Kutoa fasili zao kuhusu fasihi
|
|
2 |
Vipengele vya fasihi; Fasihi simulizi: maana yake, tanzu na vipera vyake;
|
Maana ya fasihi simulizi
Tanzu na vipera vya fasihi simulizi |
LENGO 4 |
Mawasiliano na ushirikiano(wanapojadiliana kuhusu tanzu na vipera vya fasihi |
Kuwaeleza wanafunzi kuhusu tanzu na vipera vya fasihi simulizi |
Wanafunzi kujadilina kufafanua tanzu na vipera vya fasihi simulizi |
|
3 |
Fasihi andishi:Riwaya
|
Maana ya riwaya, Historia ya riwaya Aina za riwaya |
LENGO 4 |
Ufanisi wa kibinafsi(wanapoeleza maana ya riwaya na historia yake na aina za riwaya |
Kueleza maana ya riwaya na historia yake |
Wanafunzi kueleza maana ya riwaya Wanafunzi kutafiti mtandaoni kuhusu historia ya riwaya na aina za riwaya |
|
4 |
MUJARABU WA KWANZA(KAZI YA KIBINAFSI-10% |
|
|
Kufikiri kwa makini na kutatua matatizo, mawazo (mwanafunzi anapojibu maswali) |
|
|
|
5 |
Fasihi andishi:Riwaya
|
Fani na maudhui katika riwaya/dhamira, uchambuzi wa riwaya
|
LENGO 4,6 |
Ujuzi wa kidijitali (kutafuta mtandaoni fani na maudhui katika riwaya ) |
Kueleza fani na maudhui katika riwaya |
Wanafunzi kujadili vipengele vya kuzingatiwa katika uchambuzi wa riwaya
Kuandika |
|
6 |
Hadithi fupi |
Maana ya hadithi fupi, fani na maudhui
|
LENGO 4,6 |
Mawasiliano na ushirikiano(wanapoeleza maana ya hadithi fupi na kuichambua) |
Kuuliza maswali
|
Wanafunzi kusoma na kuchambua hadithi fupi |
|
7 |
Tamthilia |
Maana ya tamthilia, historia ya tamthilia, uhakiki wa tamthilia |
LENGO 4,6 |
Mawasiliano na ushirikiano(wanapoeleza maana na historia ya tamthilia)
Ubunifu(wanapochambua tamthilia) |
Kuwaelekeza wanafunzi katika kueleza historia ya tamthilia na uhakiki wake) |
Wanafunzi kueleza maana ya tamthilia na historia yake
Wanafunzi kuhakiki tamthilia |
|
8 |
MUJARABU WA PILI (MAKUNDI NA UWASILISHAJI)- 10%
|
|
|
Mawasiliano na ushirikiano, ujuzi wa kidijitali,ubunifu, kufikiri na kutatua matatizo |
|
|
|
9 |
Ushairi
|
Maana ya ushairi, Historia ya ushairi, Aina za ushairi, Uchambuzi wa ushairi.
|
LENGO 4,6 |
Mawasiliano na ushirikiano(wanapojadiliana na kuwasilisha kuhusu ushairi) |
Kueleza maana ya ushairi, historia na aina za ushairi
|
Wanafunzi kujadiliana kuhusu historia na aina za ushairi
Wanafunzi kuchambua mashairi mbalimbali |
|
10 |
Ushairi |
Uchambuzi wa ushairi. |
LENGO 4,6 |
Mawasiliano na ushirikiano(wanapochambua mashairi mbalimbali) |
Kuchambua mashairi mbalimbali |
Wanafunzi kusoma na kuchambua mashairi mbalimbali Kuandika |
|
11 |
MAREJELEO YA KOZI |
|
|
|
|
|
|
12 |
MAREJELEO YA KOZI |
|
|
|
|
|
|
13-14
|
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA- 40% |
|
|
|
|
|
MBINU ZA KUFUNZIA
Mihadhara darasani, Majadiliano kuhusu mada mbalimbali darasani, Mawasilisho kuhusu mazoezi mbalimbali, utafiti wa maktabani na mtandaoni.
VIFAA VYA KUFUNZIA
Ubao wa kuandikia, mtandao, vitabu vya Fasihi, nakala za kusoma.
UTAHINI
Mahudhurio na Kushiriki: 10%
Mjarabu wa kwanza (wa kibinafsi) 10%
Mjarabu wa pili (Makundi na Uwasilishaji) 10%
Mjarabu wa tatu (Karatasi ya Muhula) 20%
Mjarabu wa nne (kazi ya makundi ya pili) 10%
Mtihani wa mwisho 40%
JUMLA 100%
MAKATAA
Mjarabu wa kwanza- wiki ya 4
Mjarabu wa pili(makundi na uwasilishaji)- wiki ya 8
Mjarabu wa tatu(karatasi ya muhula)- Wiki ya 9
Mjarabu wa nne (kazi ya makundi ya pili)-wiki ya 9
Mtihani wa mwisho- wiki 13-14
MAREJELEO
Abedi, K. M. (1965). Sheria za kutunga Mashairi na Diwani ya Amri. Nairobi: Kenya Literature Bureau.
Njogu, K. & Chimera, R. (1999). Ufundishaji wa Fasihi: Nadharia na Mbinu. Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation.
Wamitila, K.W. (2003). Kichocheo cha Fasihi: Simulizi na Andishi. Nairobi: Focus Books.
Wamitila, K.W. (2003). Kamusi ya Fasihi: Istilahi na Nadharia. Nairobi: Focus Books.
Wamitila, K.W. (2008). Kanzi ya Fasihi: Misingi ya Uchanganuzi wa Fasihi. Nairobi: Vide-Muwa Publishers.
